Skip to main content

Makundi 6 Ya Watu Walioko Hatarini Kupata Homa Ya Ini A (HAV)

 HOMA YA INI AINA A, ISABABISHWAYO NA HEPATITIS A

Homa hii inasababishwa na kirusi aitwae HEPATITIS A VIRUS (HAV),kumbukeni binadamu ndo kiumbe pekee ambae anaweza kubeba huyu kirusi mwilini wake (ONLY KNOWN RESORVOIR). kwa kawaida ugonjwa hauna madhara yeyote na huisha kabisa bila ya kuacha madhara ya kudumu.kiepidemiolojia ugonjwa huu upo kila sehemu duniani na kila mtu anaweza kuupata na unaweza kutokea kama mlipuko(epidemic) au kimakundi makundi(sporadic). 

NAMNA YA KUUPATA HUU UGONJWA

Njia pekee inayojulikana katika kuambukizwa maambukizi haya ni KUPITIA KULA AU KUNYWA CHAKULA,MATUNDA,MBOGA ZA MAJANI AU MAJI YENYE HUYU KIRUSI.Vile vile mama mjamzito anaweza kumuambukiza mtoto alieko tumboni ila hii ni mara chache sana kutokea. 

MAKUNDI YALIYO HATARI KUPATA HAYA MAAMBUKIZI

1) Wanaokula vyakula, matunda ambavo vipo katika mazingira ya uchafu.
2) Wanaokula mboga, samaki ambazo hazijaiva vizuri.
3) WAFUNGWA.
4) WAKIMBIZI
5) WANAJESHI
6) DAY CARE CENTERS DALILI ZAKE
Mara upatapo maambukizi haya, dalili huanza kuonekana ndani ya siku 10 hadi 50, dalili hizi hua hazieleweki eleweki(dalili mchanganyiko) na inaishaga zenyewe

Mojawapo ya dalili ambazo mgonjwa anaweza kuziona ni: -

1) kichefuchefu cha ghafla
2) kutapika
3) kuishiwa hamu ya kula.
4) Homa.
5) Mwili kuchoka choka(uchovu wa mwili mzima)
6) Maumivu ya tumbo upande wa kulia chini ya mbavu.
7) Mkojo wa njano
8) Choo cheupe kama karatasi
9) Manjano(dalili hii hutokea mwishoni)
10) kuwashwa(dalili hii hutokea mwishoni)

Jambo jema kwa maambukizi haya ni kwamba mgonjwa hataishia kupata madhara makubwa ya mwili au kifo na dalili zake huanza kuisha pale tu anapoanza kupata manjano.Vilevile mtu mwenye huu ugonjwa anaweza sana kumuambukiza mtu mwingine ndani ya siku 10-50 toka aambukizwe na uwezo huu hupotea pale anapopata manjano. 

Tuachie comment yako hapa chini kwa ushauri na maoni nasi tutafanyia kazi.

Comments

Popular posts from this blog

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...

The Interpretation of Hepatitis Viral Load Test.

What is HBV Quant.? Hepatitis B Virus - Viral Load, Quantitative test assesses the level of viral infection in the body. It measures the amount of viral DNA in the blood during the infection. Generally, this test is recommended to check the efficacy of hepatitis B treatment. Hepatitis B virus spreads mainly through body fluids or unsafe sexual intercourse. Mostly the symptoms of infection fade on their own after 4-8 weeks. However, in some cases, uncontrolled levels of HepB viral load can lead to chronic hepatitis infection and liver cirrhosis. Why is HBV Quant. done? The Hepatitis B Virus - Viral Load, Quantitative test is done: For the management of patients with chronic hepatitis B infection and currently on antiviral therapy For the diagnosis of hepatitis B for baseline values and during the course of therapy to assess the treatment response. What does HBV Quant. Measure? The Hepatitis B Virus - Viral Load, Quantitative test measures the amount of hepatitis B in a blo...

Kiungulia kwa Mama Mjamzito.

  Kiungulia ni tatizo linalosumbua idadi kubwa ya wanawake wakati wa ujauzito. Tatizo hili hutojikeza kwa mara ya kwanza wakati wa ujauzito kwa baadhi ya wanawake. Kiungulia husababishwa na asidi (tindikali) kumwagika kwenye koo la chakula kutoka kwenye tumbo la chakula. Kuna sababu nyingi zinazofanya Wajawazito kupata kiungulia mara kwa mara kuliko wanawake ambao sio wajawazito. Sababu hizo ni pamoja na Mabadiliko ya homoni yanayojitokeza wakati wa ujauzito pia mfuko wa uzazi kusukuma tumbo la chakula husababisha asidi kurudi kwenye koo la chakula Nini ufanye kuondoa au kupunguza kiungulia Tazama unachokula vyakula vyenye tindikali na vile vichachu ni chanzo cha asidi nyingi tumboni. Punguza vyakula na matunda machachu, nyanya, vitunguu maji, kahawa na chai nyeusi, chokleti, soda ,tangawizi na vyakula vilivyokaangwa kama chips. Kula Mara nyingi kidogo kidogo  badala ya kula milo mikubwa mitatu katika siku Unapokula hakikisha unakaa ukiwa umenyooka  usijipinde, itasa...