Skip to main content

Makundi 6 Ya Watu Walioko Hatarini Kupata Homa Ya Ini A (HAV)

 HOMA YA INI AINA A, ISABABISHWAYO NA HEPATITIS A

Homa hii inasababishwa na kirusi aitwae HEPATITIS A VIRUS (HAV),kumbukeni binadamu ndo kiumbe pekee ambae anaweza kubeba huyu kirusi mwilini wake (ONLY KNOWN RESORVOIR). kwa kawaida ugonjwa hauna madhara yeyote na huisha kabisa bila ya kuacha madhara ya kudumu.kiepidemiolojia ugonjwa huu upo kila sehemu duniani na kila mtu anaweza kuupata na unaweza kutokea kama mlipuko(epidemic) au kimakundi makundi(sporadic). 

NAMNA YA KUUPATA HUU UGONJWA

Njia pekee inayojulikana katika kuambukizwa maambukizi haya ni KUPITIA KULA AU KUNYWA CHAKULA,MATUNDA,MBOGA ZA MAJANI AU MAJI YENYE HUYU KIRUSI.Vile vile mama mjamzito anaweza kumuambukiza mtoto alieko tumboni ila hii ni mara chache sana kutokea. 

MAKUNDI YALIYO HATARI KUPATA HAYA MAAMBUKIZI

1) Wanaokula vyakula, matunda ambavo vipo katika mazingira ya uchafu.
2) Wanaokula mboga, samaki ambazo hazijaiva vizuri.
3) WAFUNGWA.
4) WAKIMBIZI
5) WANAJESHI
6) DAY CARE CENTERS DALILI ZAKE
Mara upatapo maambukizi haya, dalili huanza kuonekana ndani ya siku 10 hadi 50, dalili hizi hua hazieleweki eleweki(dalili mchanganyiko) na inaishaga zenyewe

Mojawapo ya dalili ambazo mgonjwa anaweza kuziona ni: -

1) kichefuchefu cha ghafla
2) kutapika
3) kuishiwa hamu ya kula.
4) Homa.
5) Mwili kuchoka choka(uchovu wa mwili mzima)
6) Maumivu ya tumbo upande wa kulia chini ya mbavu.
7) Mkojo wa njano
8) Choo cheupe kama karatasi
9) Manjano(dalili hii hutokea mwishoni)
10) kuwashwa(dalili hii hutokea mwishoni)

Jambo jema kwa maambukizi haya ni kwamba mgonjwa hataishia kupata madhara makubwa ya mwili au kifo na dalili zake huanza kuisha pale tu anapoanza kupata manjano.Vilevile mtu mwenye huu ugonjwa anaweza sana kumuambukiza mtu mwingine ndani ya siku 10-50 toka aambukizwe na uwezo huu hupotea pale anapopata manjano. 

Tuachie comment yako hapa chini kwa ushauri na maoni nasi tutafanyia kazi.

Comments

Popular posts from this blog

Hawa Hapa Maadui 3 Wakubwa wa Homa ya Ini.

Hapa swali kubwa kabisaa linaulizwa ni kitu gani mtu mwenye Homa ya ini hatakiwi kutumia?  Kabla sijataja vitu hivo nawakumbusha tu kua "kua karibu na Mungu". kuna mambo mengi mnoo ya kutokufanya kama mtu unaugojwa wa ini, kiasi ambacho tukikwambia kila kitu utakata tamaa, lakini leo tunakupa mambo matatu tu yakutokufanya na hapa ni kwa maana njema ya kuilinda afya na mwonekano wa mwili wako.  Haya sasa 1. Achana kabisaa na nyama nyekundu yaani ya mbuzi, ya ng'ombe na wanyama wa porini. wazee wa zamani nyama hawakula fresh meat, walikua wanabanika inakauka  ili kutoa maji na sumu kwenye hiyo nyama. vijana wa leo tunaweza tunajivunia kula vizuri lakini tunakula sumu nyningi sana bila kujua, acha kula nyama nyekundu. 2. Vinywaji kama vile Pombe na vitu vyenye asili ya pombe namanisha pombe yenyewe na wine, soda na energy drinks acha kabisaa  3. Punguza kufanya tendo la ndoa. Hasa wanaume Kama umeoa punguza kwa maana ya kwamba kuna siku zingine "kichwa cha nyumba" ...

DALILI 13 ZA MTU MWENYE HOMA YA INI (CHRONIC VIRAL HEPATITIS)

  HATUA YA PILI YA MAAMBUKIZI YA HBV NA YA MUDA MREFU (CHRONIC HEPATITIS B HBV) Hii ndio hatua ambayo wagonjwa wengi huanza kuonyesha dalili kubwa ama madhara makubwa yatokanayo na maambukizi ya HBV. Katika hatua hii mgonjwa anakua ameshapata madhara makubwa na ya kudumu,yaani mgonjwa anakua anaumwa kwelikweli.Ikumbukwe kuna baadhi ya watu hawaoni dalili yoyote kwa hiyo wanakuja kujishtukia wameshapata madhara makubwa kama kufeli kwa ini,magonjwa ya figo,kuharibika kwa mishipa ya damu,saratani ya ini na KIFO.. Hatua hii inajumuisha madhara yahusishayo ini lenyewe (intrahepatic manifestations) na madhara yahusuyo sehemu zingine za mwili tofauti na ini(extra hepatic manifestations), baadhi ya madhara hayo ni ugonjwa wa figo(glomerular disease) na kuharibika/kushambuliwa kwa mishipa mingi ya damu katika mwili(polyarteritis nodosa) Baadhi ya dalili zionekanazo katika hatua hii ni :- 1) Kichefuchefu(nausea) 2)Kutapika(vomiting) 3) Kuishiwa ham ya kula(anorexia) 4)Homa(fever) 5)Manjano(j...

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...