Skip to main content

Jinsi Homa Ya Ini/Hepatitis Inavyomaliza Watu Wengi Bila Kujua.


 Si ajabu kuona leo neno Homa ya ini na likawa jina geni kwako, hii ni kutokana na kutofahamika kwa wengi duniani na kwa watanzia kwa ujumla. Na hapo ndo ukija kujua unatamani ungelijua toka zamani, lakini kwa kua umeliona leo hujachelewa bado.

Homa ya Ini ni ugonjwa usababishwao na virusi aina ya Hepatitis ambao husababisha mchochota wa ini na kufanya ini kupungua utendaji kazi wake hivyo kuleta kifo ama kansa ya ini.

Ugonjwa huu haujulikani na watu wengi na wengi wanaojua inawezekana alikua na ndugu yake aliepata changamoto hii au basi ni mchangia damu alipa elimu kutoka huko.

Ugonjwa huu hauna dalili za moja kwa moja na umepewa ubatizo wa jina la “Silent Killer Disease” ya kwamba ni rahisi mno ukawa na homa ya ini na usijue chochote mpka pale kinga ya mwili ikizidiwa sana na kisha kuanza kuona mabadiliko makubwa na mwili kuanza kuuma bila mpangilio wowote, mara nyingi wagonjwa wa homa ya ini hulalamika kusikia maumivu ya tumbo, mwili kuishiwa nguvu, kukosa hamu ya kula, maumivu makali upande wa kulilia kwenye ubavu pamoja na kichefuchefu na kutapika.

Kwa dalili hizi wengi hudhania ni Malaria na hapo ndo kosa kubwa linapofanyika kwani unamfanya mtu kuanza kutumia dawa ambazo hazimsaidii na zaidi anaendelea kuingia hatarini na kuwaingiza hatarini wale wanao muuguza.

Kwa taarifa ilivyo mbaya ni kwamba hapo ndo watu wengi wanaathirika kwa kua wanaowauguza hawana uelewa juu ya kujilinda zidi ya ugonjwa huu hatari hivyo inafanya maambukizi mengi kuongezeka kutokea hapa.

Na kadri mtu mmoja anaovyokaa bila kujua habari yoyote kuhusu ugonjwa huu si alie mzima wala mgonjwa basi inafanya kila mmoja kua kwenye hatari kubwa kupatwa na janga hili, watu wengi wamewaambikiza ndugu wa karibu bila kujua na walioambukizwa wakaendelea kutokujua hivyo kufanya nao wawaambukize wengine pasipo kujua.

je, unaijua hali yako ya ini?

Ndio, inatia shaka na inakufanya ujihoji uzima wako. lakini mwanzo nimesema imekusudiwa leo kuielewa changamoto hii na ufanye maamzi leo.

Ni Nini Kifanyike?

Kata mnyororo wa maambukizi kwa kuchukua uamzi wa kwenda kupima leo na kuanza kupata chanjo mara moja ili ujilinde na uwalinde wengine, chanjo inakuondolea hofu hata ukiwa kwenye vyombo vywa usafiri vya umma unakua na amani, unakua na uhuru wa kumuuguza ndugu yako hata kama akiwa na maambukizi.

Pata chanjo, Choma Chanjo leo.

Comments

Popular posts from this blog

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...

Kiungulia kwa Mama Mjamzito.

  Kiungulia ni tatizo linalosumbua idadi kubwa ya wanawake wakati wa ujauzito. Tatizo hili hutojikeza kwa mara ya kwanza wakati wa ujauzito kwa baadhi ya wanawake. Kiungulia husababishwa na asidi (tindikali) kumwagika kwenye koo la chakula kutoka kwenye tumbo la chakula. Kuna sababu nyingi zinazofanya Wajawazito kupata kiungulia mara kwa mara kuliko wanawake ambao sio wajawazito. Sababu hizo ni pamoja na Mabadiliko ya homoni yanayojitokeza wakati wa ujauzito pia mfuko wa uzazi kusukuma tumbo la chakula husababisha asidi kurudi kwenye koo la chakula Nini ufanye kuondoa au kupunguza kiungulia Tazama unachokula vyakula vyenye tindikali na vile vichachu ni chanzo cha asidi nyingi tumboni. Punguza vyakula na matunda machachu, nyanya, vitunguu maji, kahawa na chai nyeusi, chokleti, soda ,tangawizi na vyakula vilivyokaangwa kama chips. Kula Mara nyingi kidogo kidogo  badala ya kula milo mikubwa mitatu katika siku Unapokula hakikisha unakaa ukiwa umenyooka  usijipinde, itasa...

The Psychological Effect of Viral Hepatitis: Understanding the Emotional Impact

  Viral hepatitis is a global health concern affecting millions of people around the world. While the physical symptoms and medical implications of this infectious disease are widely discussed, the psychological impact often goes unnoticed. In this blog post, we will delve into the lesser-known aspect of viral hepatitis — its profound psychological effects on individuals. By shedding light on these emotional ramifications, we aim to raise awareness and promote a better understanding of the holistic impact of this condition. Fear and Anxiety: Being diagnosed with viral hepatitis can trigger intense fear and anxiety in individuals. The uncertainty surrounding the disease, its progression, and potential complications can create a sense of impending doom. The fear of transmitting the infection to loved ones or facing social stigma further exacerbates emotional distress. As a result, individuals may experience heightened anxiety, panic attacks, and a constant state of worry, impacting t...