Skip to main content

Jinsi Homa Ya Ini/Hepatitis Inavyomaliza Watu Wengi Bila Kujua.


 Si ajabu kuona leo neno Homa ya ini na likawa jina geni kwako, hii ni kutokana na kutofahamika kwa wengi duniani na kwa watanzia kwa ujumla. Na hapo ndo ukija kujua unatamani ungelijua toka zamani, lakini kwa kua umeliona leo hujachelewa bado.

Homa ya Ini ni ugonjwa usababishwao na virusi aina ya Hepatitis ambao husababisha mchochota wa ini na kufanya ini kupungua utendaji kazi wake hivyo kuleta kifo ama kansa ya ini.

Ugonjwa huu haujulikani na watu wengi na wengi wanaojua inawezekana alikua na ndugu yake aliepata changamoto hii au basi ni mchangia damu alipa elimu kutoka huko.

Ugonjwa huu hauna dalili za moja kwa moja na umepewa ubatizo wa jina la “Silent Killer Disease” ya kwamba ni rahisi mno ukawa na homa ya ini na usijue chochote mpka pale kinga ya mwili ikizidiwa sana na kisha kuanza kuona mabadiliko makubwa na mwili kuanza kuuma bila mpangilio wowote, mara nyingi wagonjwa wa homa ya ini hulalamika kusikia maumivu ya tumbo, mwili kuishiwa nguvu, kukosa hamu ya kula, maumivu makali upande wa kulilia kwenye ubavu pamoja na kichefuchefu na kutapika.

Kwa dalili hizi wengi hudhania ni Malaria na hapo ndo kosa kubwa linapofanyika kwani unamfanya mtu kuanza kutumia dawa ambazo hazimsaidii na zaidi anaendelea kuingia hatarini na kuwaingiza hatarini wale wanao muuguza.

Kwa taarifa ilivyo mbaya ni kwamba hapo ndo watu wengi wanaathirika kwa kua wanaowauguza hawana uelewa juu ya kujilinda zidi ya ugonjwa huu hatari hivyo inafanya maambukizi mengi kuongezeka kutokea hapa.

Na kadri mtu mmoja anaovyokaa bila kujua habari yoyote kuhusu ugonjwa huu si alie mzima wala mgonjwa basi inafanya kila mmoja kua kwenye hatari kubwa kupatwa na janga hili, watu wengi wamewaambikiza ndugu wa karibu bila kujua na walioambukizwa wakaendelea kutokujua hivyo kufanya nao wawaambukize wengine pasipo kujua.

je, unaijua hali yako ya ini?

Ndio, inatia shaka na inakufanya ujihoji uzima wako. lakini mwanzo nimesema imekusudiwa leo kuielewa changamoto hii na ufanye maamzi leo.

Ni Nini Kifanyike?

Kata mnyororo wa maambukizi kwa kuchukua uamzi wa kwenda kupima leo na kuanza kupata chanjo mara moja ili ujilinde na uwalinde wengine, chanjo inakuondolea hofu hata ukiwa kwenye vyombo vywa usafiri vya umma unakua na amani, unakua na uhuru wa kumuuguza ndugu yako hata kama akiwa na maambukizi.

Pata chanjo, Choma Chanjo leo.

Comments

Popular posts from this blog

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...

DALILI 13 ZA MTU MWENYE HOMA YA INI (CHRONIC VIRAL HEPATITIS)

  HATUA YA PILI YA MAAMBUKIZI YA HBV NA YA MUDA MREFU (CHRONIC HEPATITIS B HBV) Hii ndio hatua ambayo wagonjwa wengi huanza kuonyesha dalili kubwa ama madhara makubwa yatokanayo na maambukizi ya HBV. Katika hatua hii mgonjwa anakua ameshapata madhara makubwa na ya kudumu,yaani mgonjwa anakua anaumwa kwelikweli.Ikumbukwe kuna baadhi ya watu hawaoni dalili yoyote kwa hiyo wanakuja kujishtukia wameshapata madhara makubwa kama kufeli kwa ini,magonjwa ya figo,kuharibika kwa mishipa ya damu,saratani ya ini na KIFO.. Hatua hii inajumuisha madhara yahusishayo ini lenyewe (intrahepatic manifestations) na madhara yahusuyo sehemu zingine za mwili tofauti na ini(extra hepatic manifestations), baadhi ya madhara hayo ni ugonjwa wa figo(glomerular disease) na kuharibika/kushambuliwa kwa mishipa mingi ya damu katika mwili(polyarteritis nodosa) Baadhi ya dalili zionekanazo katika hatua hii ni :- 1) Kichefuchefu(nausea) 2)Kutapika(vomiting) 3) Kuishiwa ham ya kula(anorexia) 4)Homa(fever) 5)Manjano(j...

Makundi 6 Ya Watu Walioko Hatarini Kupata Homa Ya Ini A (HAV)

  HOMA YA INI AINA A, ISABABISHWAYO NA HEPATITIS A Homa hii inasababishwa na kirusi aitwae HEPATITIS A VIRUS (HAV),kumbukeni binadamu ndo kiumbe pekee ambae anaweza kubeba huyu kirusi mwilini wake (ONLY KNOWN RESORVOIR). kwa kawaida ugonjwa hauna madhara yeyote na huisha kabisa bila ya kuacha madhara ya kudumu.kiepidemiolojia ugonjwa huu upo kila sehemu duniani na kila mtu anaweza kuupata na unaweza kutokea kama mlipuko(epidemic) au kimakundi makundi(sporadic).  NAMNA YA KUUPATA HUU UGONJWA Njia pekee inayojulikana katika kuambukizwa maambukizi haya ni KUPITIA KULA AU KUNYWA CHAKULA,MATUNDA,MBOGA ZA MAJANI AU MAJI YENYE HUYU KIRUSI.Vile vile mama mjamzito anaweza kumuambukiza mtoto alieko tumboni ila hii ni mara chache sana kutokea.  MAKUNDI YALIYO HATARI KUPATA HAYA MAAMBUKIZI 1) Wanaokula vyakula, matunda ambavo vipo katika mazingira ya uchafu. 2) Wanaokula mboga, samaki ambazo hazijaiva vizuri. 3) WAFUNGWA. 4) WAKIMBIZI 5) WANAJESHI 6) DAY CARE CENTERS DALILI ZAKE Mara...