Skip to main content

Kiungulia kwa Mama Mjamzito.


 Kiungulia ni tatizo linalosumbua idadi kubwa ya wanawake wakati wa ujauzito. Tatizo hili hutojikeza kwa mara ya kwanza wakati wa ujauzito kwa baadhi ya wanawake.

Kiungulia husababishwa na asidi (tindikali) kumwagika kwenye koo la chakula kutoka kwenye tumbo la chakula.

Kuna sababu nyingi zinazofanya Wajawazito kupata kiungulia mara kwa mara kuliko wanawake ambao sio wajawazito. Sababu hizo ni pamoja na Mabadiliko ya homoni yanayojitokeza wakati wa ujauzito pia mfuko wa uzazi kusukuma tumbo la chakula husababisha asidi kurudi kwenye koo la chakula

Nini ufanye kuondoa au kupunguza kiungulia

Tazama unachokula
vyakula vyenye tindikali na vile vichachu ni chanzo cha asidi nyingi tumboni. Punguza vyakula na matunda machachu, nyanya, vitunguu maji, kahawa na chai nyeusi, chokleti, soda ,tangawizi na vyakula vilivyokaangwa kama chips.

Kula Mara nyingi kidogo kidogo badala ya kula milo mikubwa mitatu katika siku

Unapokula hakikisha unakaa ukiwa umenyooka usijipinde, itasaidia chakula kuteremka vizuri tumboni.

Masaa matatu kuelekea kulala usile chakula. Unapolala yatakiwa kuwe hakuna chakula tumboni itakusaidia kukontroo kiungulia .

Usivute Sigara: Kemikali zilizopo kwenye sigara zinafanya kulegea kwa valve zinazouzia chakula kutoka.

Unapolala hakikisha unaweka mto: Hakikisha unapoenda kulala eneo la juu la kichwa linakuwa juu kidogo.

Vaa nguo pana zisizobana

Kunywa maji baada ya kumaliza kula na siyo katikati ya mlo

Usitumie pombe: Pombe ni mbaya hata kwa ukuaji wa mtoto maana hupelekea mtoto kuwa na ulemavu wa ubongo na viungo. Pombe pia hufanya valve za kwenye koo la chakula kulegea na hivo kuruusu chakula kurudi juu.

Muone Daktari: Hali ikiwa mbaya hakikisha unaenda hospitali, kwa kulingana na hali yako ya ujauzito, daktari atapendekeza dawa za kukupatia. Usimeze dawa bila kupata ushauri wa daktari maana zinaweza kukudhuru.

 


Comments

Popular posts from this blog

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...

The Psychological Effect of Viral Hepatitis: Understanding the Emotional Impact

  Viral hepatitis is a global health concern affecting millions of people around the world. While the physical symptoms and medical implications of this infectious disease are widely discussed, the psychological impact often goes unnoticed. In this blog post, we will delve into the lesser-known aspect of viral hepatitis — its profound psychological effects on individuals. By shedding light on these emotional ramifications, we aim to raise awareness and promote a better understanding of the holistic impact of this condition. Fear and Anxiety: Being diagnosed with viral hepatitis can trigger intense fear and anxiety in individuals. The uncertainty surrounding the disease, its progression, and potential complications can create a sense of impending doom. The fear of transmitting the infection to loved ones or facing social stigma further exacerbates emotional distress. As a result, individuals may experience heightened anxiety, panic attacks, and a constant state of worry, impacting t...