Skip to main content

Kiungulia kwa Mama Mjamzito.


 Kiungulia ni tatizo linalosumbua idadi kubwa ya wanawake wakati wa ujauzito. Tatizo hili hutojikeza kwa mara ya kwanza wakati wa ujauzito kwa baadhi ya wanawake.

Kiungulia husababishwa na asidi (tindikali) kumwagika kwenye koo la chakula kutoka kwenye tumbo la chakula.

Kuna sababu nyingi zinazofanya Wajawazito kupata kiungulia mara kwa mara kuliko wanawake ambao sio wajawazito. Sababu hizo ni pamoja na Mabadiliko ya homoni yanayojitokeza wakati wa ujauzito pia mfuko wa uzazi kusukuma tumbo la chakula husababisha asidi kurudi kwenye koo la chakula

Nini ufanye kuondoa au kupunguza kiungulia

Tazama unachokula
vyakula vyenye tindikali na vile vichachu ni chanzo cha asidi nyingi tumboni. Punguza vyakula na matunda machachu, nyanya, vitunguu maji, kahawa na chai nyeusi, chokleti, soda ,tangawizi na vyakula vilivyokaangwa kama chips.

Kula Mara nyingi kidogo kidogo badala ya kula milo mikubwa mitatu katika siku

Unapokula hakikisha unakaa ukiwa umenyooka usijipinde, itasaidia chakula kuteremka vizuri tumboni.

Masaa matatu kuelekea kulala usile chakula. Unapolala yatakiwa kuwe hakuna chakula tumboni itakusaidia kukontroo kiungulia .

Usivute Sigara: Kemikali zilizopo kwenye sigara zinafanya kulegea kwa valve zinazouzia chakula kutoka.

Unapolala hakikisha unaweka mto: Hakikisha unapoenda kulala eneo la juu la kichwa linakuwa juu kidogo.

Vaa nguo pana zisizobana

Kunywa maji baada ya kumaliza kula na siyo katikati ya mlo

Usitumie pombe: Pombe ni mbaya hata kwa ukuaji wa mtoto maana hupelekea mtoto kuwa na ulemavu wa ubongo na viungo. Pombe pia hufanya valve za kwenye koo la chakula kulegea na hivo kuruusu chakula kurudi juu.

Muone Daktari: Hali ikiwa mbaya hakikisha unaenda hospitali, kwa kulingana na hali yako ya ujauzito, daktari atapendekeza dawa za kukupatia. Usimeze dawa bila kupata ushauri wa daktari maana zinaweza kukudhuru.

 


Comments

Popular posts from this blog

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...

The Interpretation of Hepatitis Viral Load Test.

What is HBV Quant.? Hepatitis B Virus - Viral Load, Quantitative test assesses the level of viral infection in the body. It measures the amount of viral DNA in the blood during the infection. Generally, this test is recommended to check the efficacy of hepatitis B treatment. Hepatitis B virus spreads mainly through body fluids or unsafe sexual intercourse. Mostly the symptoms of infection fade on their own after 4-8 weeks. However, in some cases, uncontrolled levels of HepB viral load can lead to chronic hepatitis infection and liver cirrhosis. Why is HBV Quant. done? The Hepatitis B Virus - Viral Load, Quantitative test is done: For the management of patients with chronic hepatitis B infection and currently on antiviral therapy For the diagnosis of hepatitis B for baseline values and during the course of therapy to assess the treatment response. What does HBV Quant. Measure? The Hepatitis B Virus - Viral Load, Quantitative test measures the amount of hepatitis B in a blo...