Skip to main content

Kiungulia kwa Mama Mjamzito.


 Kiungulia ni tatizo linalosumbua idadi kubwa ya wanawake wakati wa ujauzito. Tatizo hili hutojikeza kwa mara ya kwanza wakati wa ujauzito kwa baadhi ya wanawake.

Kiungulia husababishwa na asidi (tindikali) kumwagika kwenye koo la chakula kutoka kwenye tumbo la chakula.

Kuna sababu nyingi zinazofanya Wajawazito kupata kiungulia mara kwa mara kuliko wanawake ambao sio wajawazito. Sababu hizo ni pamoja na Mabadiliko ya homoni yanayojitokeza wakati wa ujauzito pia mfuko wa uzazi kusukuma tumbo la chakula husababisha asidi kurudi kwenye koo la chakula

Nini ufanye kuondoa au kupunguza kiungulia

Tazama unachokula
vyakula vyenye tindikali na vile vichachu ni chanzo cha asidi nyingi tumboni. Punguza vyakula na matunda machachu, nyanya, vitunguu maji, kahawa na chai nyeusi, chokleti, soda ,tangawizi na vyakula vilivyokaangwa kama chips.

Kula Mara nyingi kidogo kidogo badala ya kula milo mikubwa mitatu katika siku

Unapokula hakikisha unakaa ukiwa umenyooka usijipinde, itasaidia chakula kuteremka vizuri tumboni.

Masaa matatu kuelekea kulala usile chakula. Unapolala yatakiwa kuwe hakuna chakula tumboni itakusaidia kukontroo kiungulia .

Usivute Sigara: Kemikali zilizopo kwenye sigara zinafanya kulegea kwa valve zinazouzia chakula kutoka.

Unapolala hakikisha unaweka mto: Hakikisha unapoenda kulala eneo la juu la kichwa linakuwa juu kidogo.

Vaa nguo pana zisizobana

Kunywa maji baada ya kumaliza kula na siyo katikati ya mlo

Usitumie pombe: Pombe ni mbaya hata kwa ukuaji wa mtoto maana hupelekea mtoto kuwa na ulemavu wa ubongo na viungo. Pombe pia hufanya valve za kwenye koo la chakula kulegea na hivo kuruusu chakula kurudi juu.

Muone Daktari: Hali ikiwa mbaya hakikisha unaenda hospitali, kwa kulingana na hali yako ya ujauzito, daktari atapendekeza dawa za kukupatia. Usimeze dawa bila kupata ushauri wa daktari maana zinaweza kukudhuru.

 


Comments

Popular posts from this blog

Hawa Hapa Maadui 3 Wakubwa wa Homa ya Ini.

Hapa swali kubwa kabisaa linaulizwa ni kitu gani mtu mwenye Homa ya ini hatakiwi kutumia?  Kabla sijataja vitu hivo nawakumbusha tu kua "kua karibu na Mungu". kuna mambo mengi mnoo ya kutokufanya kama mtu unaugojwa wa ini, kiasi ambacho tukikwambia kila kitu utakata tamaa, lakini leo tunakupa mambo matatu tu yakutokufanya na hapa ni kwa maana njema ya kuilinda afya na mwonekano wa mwili wako.  Haya sasa 1. Achana kabisaa na nyama nyekundu yaani ya mbuzi, ya ng'ombe na wanyama wa porini. wazee wa zamani nyama hawakula fresh meat, walikua wanabanika inakauka  ili kutoa maji na sumu kwenye hiyo nyama. vijana wa leo tunaweza tunajivunia kula vizuri lakini tunakula sumu nyningi sana bila kujua, acha kula nyama nyekundu. 2. Vinywaji kama vile Pombe na vitu vyenye asili ya pombe namanisha pombe yenyewe na wine, soda na energy drinks acha kabisaa  3. Punguza kufanya tendo la ndoa. Hasa wanaume Kama umeoa punguza kwa maana ya kwamba kuna siku zingine "kichwa cha nyumba" ...

DALILI 13 ZA MTU MWENYE HOMA YA INI (CHRONIC VIRAL HEPATITIS)

  HATUA YA PILI YA MAAMBUKIZI YA HBV NA YA MUDA MREFU (CHRONIC HEPATITIS B HBV) Hii ndio hatua ambayo wagonjwa wengi huanza kuonyesha dalili kubwa ama madhara makubwa yatokanayo na maambukizi ya HBV. Katika hatua hii mgonjwa anakua ameshapata madhara makubwa na ya kudumu,yaani mgonjwa anakua anaumwa kwelikweli.Ikumbukwe kuna baadhi ya watu hawaoni dalili yoyote kwa hiyo wanakuja kujishtukia wameshapata madhara makubwa kama kufeli kwa ini,magonjwa ya figo,kuharibika kwa mishipa ya damu,saratani ya ini na KIFO.. Hatua hii inajumuisha madhara yahusishayo ini lenyewe (intrahepatic manifestations) na madhara yahusuyo sehemu zingine za mwili tofauti na ini(extra hepatic manifestations), baadhi ya madhara hayo ni ugonjwa wa figo(glomerular disease) na kuharibika/kushambuliwa kwa mishipa mingi ya damu katika mwili(polyarteritis nodosa) Baadhi ya dalili zionekanazo katika hatua hii ni :- 1) Kichefuchefu(nausea) 2)Kutapika(vomiting) 3) Kuishiwa ham ya kula(anorexia) 4)Homa(fever) 5)Manjano(j...

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...