Skip to main content

Jinsi Wanajeshi/Askari Wanavyoambukizwa Homa ya Ini.

 


Pamoja na uzuri wa kazi hii na majukumu ya jeshi lolote katika nchi kua ni mhimu sana katika kuhakikisha usalama wa nchi, lakini kundi hili ni moja ya makundi sensitive kwenye ugonjwa wa hepatitis.


Kutokana na mazingira ya kazi yao kua ni mazoezi yanayotoa jasho, kupata michubuko na kuishi kwa pamoja kwa wingi inawaweka kwenye hatari ya hepatitis kuenea kwa kasi endapo tu kuna mmoja kati yao ameathirika.

Na endapo akigundurika kua na shida hii mwanajeshi huzikosa fursa nyingi mnoo kiasi ambacho anaweza kuona hamna umaana wa kua mwanajeshi kwani mda wote atahesabika kua ni mgonjwa.

HASARA ANAZOZIPATA MWANAJESHI AU ASKARI BAADA YA KUPATA MAAMBUKIZI YA HOMA YA INI
1. Hawezi kwenda kusoma course.
2. Hawezi kwenda nje ya nchi kwenye majukumu ya kikazi.
3. Hawezi kufanyishwa mazoezi makali ya kumpanua uwezo wake.  

Itoshe kusema anakuwepo tu yani, anakua mwanajeshi jina tu, na kwa kua wanajeshi wengi wanapenda kazi zao na fursa walizonazo basi ikitokea kakosa hizo fursa kisaikolojia hawezi kua sawa.

Basi kama una ndugu yako mwanajeshi ni vizuri mpe hii habari, afanye uchunguzi apate kujua afya yake ya ini, kujua mapema kunasaidia sana 

1. Inakuondolea panic mfano wakiwa wanapima kwa ajili ya kwenda course mara ghafla aambiwe anatatizo la hepatitis kwakweli inasumbua akilini sana. 
2. Lakini pia inakufanya kubadili life stlye mapema ili usiendelee kulihatarisha ini. 
3. kuiepusha familia yako isipate maambukizi ya homa ya ini kwa kuipeleka kupata chanjo.

Inakufanya kutafuta utatuzi mapema kabisaa kabla ya kuathirika zaidi na unapunguza matumizi ya dawa kwa mda mrefu kwasababu unakua umewahi mapemaaa 

Ndugu zetu tuwatumie hii habari wachukue chanjo ili kuepuka na hili tatizo.

Comments

Popular posts from this blog

Hawa Hapa Maadui 3 Wakubwa wa Homa ya Ini.

Hapa swali kubwa kabisaa linaulizwa ni kitu gani mtu mwenye Homa ya ini hatakiwi kutumia?  Kabla sijataja vitu hivo nawakumbusha tu kua "kua karibu na Mungu". kuna mambo mengi mnoo ya kutokufanya kama mtu unaugojwa wa ini, kiasi ambacho tukikwambia kila kitu utakata tamaa, lakini leo tunakupa mambo matatu tu yakutokufanya na hapa ni kwa maana njema ya kuilinda afya na mwonekano wa mwili wako.  Haya sasa 1. Achana kabisaa na nyama nyekundu yaani ya mbuzi, ya ng'ombe na wanyama wa porini. wazee wa zamani nyama hawakula fresh meat, walikua wanabanika inakauka  ili kutoa maji na sumu kwenye hiyo nyama. vijana wa leo tunaweza tunajivunia kula vizuri lakini tunakula sumu nyningi sana bila kujua, acha kula nyama nyekundu. 2. Vinywaji kama vile Pombe na vitu vyenye asili ya pombe namanisha pombe yenyewe na wine, soda na energy drinks acha kabisaa  3. Punguza kufanya tendo la ndoa. Hasa wanaume Kama umeoa punguza kwa maana ya kwamba kuna siku zingine "kichwa cha nyumba" ...

DALILI 13 ZA MTU MWENYE HOMA YA INI (CHRONIC VIRAL HEPATITIS)

  HATUA YA PILI YA MAAMBUKIZI YA HBV NA YA MUDA MREFU (CHRONIC HEPATITIS B HBV) Hii ndio hatua ambayo wagonjwa wengi huanza kuonyesha dalili kubwa ama madhara makubwa yatokanayo na maambukizi ya HBV. Katika hatua hii mgonjwa anakua ameshapata madhara makubwa na ya kudumu,yaani mgonjwa anakua anaumwa kwelikweli.Ikumbukwe kuna baadhi ya watu hawaoni dalili yoyote kwa hiyo wanakuja kujishtukia wameshapata madhara makubwa kama kufeli kwa ini,magonjwa ya figo,kuharibika kwa mishipa ya damu,saratani ya ini na KIFO.. Hatua hii inajumuisha madhara yahusishayo ini lenyewe (intrahepatic manifestations) na madhara yahusuyo sehemu zingine za mwili tofauti na ini(extra hepatic manifestations), baadhi ya madhara hayo ni ugonjwa wa figo(glomerular disease) na kuharibika/kushambuliwa kwa mishipa mingi ya damu katika mwili(polyarteritis nodosa) Baadhi ya dalili zionekanazo katika hatua hii ni :- 1) Kichefuchefu(nausea) 2)Kutapika(vomiting) 3) Kuishiwa ham ya kula(anorexia) 4)Homa(fever) 5)Manjano(j...

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...