Skip to main content

UTAFANYA NINI UKIGUNDUA KUA MWENZI/MPENZI WAKO ANA MAAMBUKIZI YA HOMA YA INI?



Kwanza naanza Kwa kutoa hongera Kwa wote wanao ishi na wenzi wao wenye maambukizi.


Pili naelewa ilivyo changamoto Kwa mwanaume kumweleza mke kua anachangamoto hii, ni kutokana na wanawake wengi kujua kua kupata hepatitis inatokana na kuchepuka tu na Hali hii ni tofauti Kwa yeye mke anaweza tumia kigezo Cha wakati wa kujifungua. Lakini ukweli ni kwamba Kila mtu Yuko kwenye hatari ya kupata maambuki mpka tu uchanje.

MISINGI YA NDOA
Wakati wa kufunga ndoa Kuna kiapo japo hatuishi Kwa kiapo tunaishi Kwa Upendo. MISINGI ya ndoa ni kuvumiliana, kusameheana, kupendana, kushauriana na kulekebishana na SI kusimangana, kufukuzana, kutengana wala kuvulugana.

Kipimo Cha Imani; MAJARIBU..

Sasa inapotokea Kati yenu ana homa ya ini zingatia MISINGI ya ndoa na kipimo Cha Imani, yaani huwezi kujua unampenda kiasi Gani mpka utakapojaribiwa na kubaki kwenye Msingi wa kuvumiliana... Umenielewa ??
Ni hivi...Kama mtu amepata hii changamoto uko nae then akuambie kua anahili tatizo na uamue kumwacha basi jua kabisaa kwamba hata kama uliwahi kutamka "I love you "x1000 basi zinakua Haina maana.

kingine ni kwamba ukimkuta mwenza wako anatatizo na wewe ni mzima we mshukru Mungu tu maana hata wewe hukua na ujanja wa kulikwepa ila Mungu tu. Na pengine ukipata hii shida baada ya kujua pengine Hofu Yako ndo itakua imekupelekea kupata.

Sasa, mkishajua MWENZI wako ana tatizo basi nenda kapime Kisha Anza chanjo huku mkichukua tahadhari ya namna ya kushiriki tendo la ndoa Kwa maana ya kutumia Kinga katika kipindi Cha wewe ukiwa unapata chanjo na baada ya hapo maisha yanarudi kawaida kufurahia unganiko lenu katika nyama😊.
Hili jaribu mkilivuka Kwa kusimama nae, baada ya hapo MWENZI wako atakuheshimu mnoo na niamini Mimi kwamba atakupenda mno labda tu awe mjinga mjinga.
Asante.

Comments

Popular posts from this blog

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...

DALILI 13 ZA MTU MWENYE HOMA YA INI (CHRONIC VIRAL HEPATITIS)

  HATUA YA PILI YA MAAMBUKIZI YA HBV NA YA MUDA MREFU (CHRONIC HEPATITIS B HBV) Hii ndio hatua ambayo wagonjwa wengi huanza kuonyesha dalili kubwa ama madhara makubwa yatokanayo na maambukizi ya HBV. Katika hatua hii mgonjwa anakua ameshapata madhara makubwa na ya kudumu,yaani mgonjwa anakua anaumwa kwelikweli.Ikumbukwe kuna baadhi ya watu hawaoni dalili yoyote kwa hiyo wanakuja kujishtukia wameshapata madhara makubwa kama kufeli kwa ini,magonjwa ya figo,kuharibika kwa mishipa ya damu,saratani ya ini na KIFO.. Hatua hii inajumuisha madhara yahusishayo ini lenyewe (intrahepatic manifestations) na madhara yahusuyo sehemu zingine za mwili tofauti na ini(extra hepatic manifestations), baadhi ya madhara hayo ni ugonjwa wa figo(glomerular disease) na kuharibika/kushambuliwa kwa mishipa mingi ya damu katika mwili(polyarteritis nodosa) Baadhi ya dalili zionekanazo katika hatua hii ni :- 1) Kichefuchefu(nausea) 2)Kutapika(vomiting) 3) Kuishiwa ham ya kula(anorexia) 4)Homa(fever) 5)Manjano(j...

Makundi 6 Ya Watu Walioko Hatarini Kupata Homa Ya Ini A (HAV)

  HOMA YA INI AINA A, ISABABISHWAYO NA HEPATITIS A Homa hii inasababishwa na kirusi aitwae HEPATITIS A VIRUS (HAV),kumbukeni binadamu ndo kiumbe pekee ambae anaweza kubeba huyu kirusi mwilini wake (ONLY KNOWN RESORVOIR). kwa kawaida ugonjwa hauna madhara yeyote na huisha kabisa bila ya kuacha madhara ya kudumu.kiepidemiolojia ugonjwa huu upo kila sehemu duniani na kila mtu anaweza kuupata na unaweza kutokea kama mlipuko(epidemic) au kimakundi makundi(sporadic).  NAMNA YA KUUPATA HUU UGONJWA Njia pekee inayojulikana katika kuambukizwa maambukizi haya ni KUPITIA KULA AU KUNYWA CHAKULA,MATUNDA,MBOGA ZA MAJANI AU MAJI YENYE HUYU KIRUSI.Vile vile mama mjamzito anaweza kumuambukiza mtoto alieko tumboni ila hii ni mara chache sana kutokea.  MAKUNDI YALIYO HATARI KUPATA HAYA MAAMBUKIZI 1) Wanaokula vyakula, matunda ambavo vipo katika mazingira ya uchafu. 2) Wanaokula mboga, samaki ambazo hazijaiva vizuri. 3) WAFUNGWA. 4) WAKIMBIZI 5) WANAJESHI 6) DAY CARE CENTERS DALILI ZAKE Mara...