Skip to main content

JE, UNAFAHAMU KUA UNAWEZA KUFA NDANI YA MASAA 24 TU KWA HUU UGONJWA?

Hii ni sitori ya hepatitis ambayo pamoja na kwamba unaweza kupuuzia kuchoma chanjo, pamoja na kwamba unaweza kukaa mda mrefu nao hadi mpka miaka 20, pamoja kwamba wakati mwingine huoni dalili kabisaa, lakini kwenye Hepatitis B kwa watu wachache sana wanaweza kufa kwa mda mfupi sana.

Sasa katika homa zote za ini, homa inayosababishwa na huyu kirusi ndo hatari kushinda wote na ndo gumzo dunia nzima kwani kirusi huyu anahusika na kutokea kwa madhara mengi na makubwa ikiwemo KIFO.

Kitakwimu dunia inakadiriwa kua na watu MILIONI 248 wanaoishi na hawa virusi wa HBV na inakadiriwa pia watu wapatao 600000 HUPOTEZA MAISHA KILA MWAKA kutokana na madhara ya HBV kwa ini na sehemu zingine za mwili. Kwa kweli hili ni janga kwa taifa na dunia kwa ujumla.

Nimshukuru tu Mungu kwani kwa sasa kuna chanjo nzuri dhidi ya HBV. Chanjo hii imepunguza sana maambukizi ya HBV na kwa maana hiyo vifo na madhara mengine yatokanayo na HBV yamepungua.

Niwaambie tena maambukizi ya HBV yapo sana na watu hawajijui na huyu kirusi anaweza kukuua ndani ya saa 24!!!!(fulminant hepatitis), fulminant hepatitis huambana na kufeli kwa ini na kisha mwili kuzidiwa na sumu. Ni mbaya kuliko HIV....jihadharini sana. .

Ubaya mwingine wa huyu kirusi hua anasababisha madhara makubwa na ana hatua au nyakati mbili..

1.Hua ana hatua za awali(acute hepatitis) na .
2. Hatua za baadae/muda mrefu(chronic hepatitis), hii hatua ya muda mrefu ndo mbaya Zaidi kwani inapelekea mgonjwa kupata madhara makubwa ya ini kama ini kushindwa kufanya kazi,  vivimbe kwenye ini(liver cirrhosis), saratani ya ini(hepatocellular carcinoma) na KIFO, itoshe kusema tu kua chanjo ni suruhisho la homa ya ini, kadri unavyochelewa kupata chanjo ya homa ya ini ndo unaendelea kijiweka hatarini zaidi.

Je, umechoma chanjo? unasubiri nini?

Comments

Popular posts from this blog

Hawa Hapa Maadui 3 Wakubwa wa Homa ya Ini.

Hapa swali kubwa kabisaa linaulizwa ni kitu gani mtu mwenye Homa ya ini hatakiwi kutumia?  Kabla sijataja vitu hivo nawakumbusha tu kua "kua karibu na Mungu". kuna mambo mengi mnoo ya kutokufanya kama mtu unaugojwa wa ini, kiasi ambacho tukikwambia kila kitu utakata tamaa, lakini leo tunakupa mambo matatu tu yakutokufanya na hapa ni kwa maana njema ya kuilinda afya na mwonekano wa mwili wako.  Haya sasa 1. Achana kabisaa na nyama nyekundu yaani ya mbuzi, ya ng'ombe na wanyama wa porini. wazee wa zamani nyama hawakula fresh meat, walikua wanabanika inakauka  ili kutoa maji na sumu kwenye hiyo nyama. vijana wa leo tunaweza tunajivunia kula vizuri lakini tunakula sumu nyningi sana bila kujua, acha kula nyama nyekundu. 2. Vinywaji kama vile Pombe na vitu vyenye asili ya pombe namanisha pombe yenyewe na wine, soda na energy drinks acha kabisaa  3. Punguza kufanya tendo la ndoa. Hasa wanaume Kama umeoa punguza kwa maana ya kwamba kuna siku zingine "kichwa cha nyumba" ...

DALILI 13 ZA MTU MWENYE HOMA YA INI (CHRONIC VIRAL HEPATITIS)

  HATUA YA PILI YA MAAMBUKIZI YA HBV NA YA MUDA MREFU (CHRONIC HEPATITIS B HBV) Hii ndio hatua ambayo wagonjwa wengi huanza kuonyesha dalili kubwa ama madhara makubwa yatokanayo na maambukizi ya HBV. Katika hatua hii mgonjwa anakua ameshapata madhara makubwa na ya kudumu,yaani mgonjwa anakua anaumwa kwelikweli.Ikumbukwe kuna baadhi ya watu hawaoni dalili yoyote kwa hiyo wanakuja kujishtukia wameshapata madhara makubwa kama kufeli kwa ini,magonjwa ya figo,kuharibika kwa mishipa ya damu,saratani ya ini na KIFO.. Hatua hii inajumuisha madhara yahusishayo ini lenyewe (intrahepatic manifestations) na madhara yahusuyo sehemu zingine za mwili tofauti na ini(extra hepatic manifestations), baadhi ya madhara hayo ni ugonjwa wa figo(glomerular disease) na kuharibika/kushambuliwa kwa mishipa mingi ya damu katika mwili(polyarteritis nodosa) Baadhi ya dalili zionekanazo katika hatua hii ni :- 1) Kichefuchefu(nausea) 2)Kutapika(vomiting) 3) Kuishiwa ham ya kula(anorexia) 4)Homa(fever) 5)Manjano(j...

Fahamu Kuhusu Matibabu, Kinga na Makundi Maalumu Yanayostahili Kinga ya Hepatitis A.

MATIBABU YAKE (HAV).  Ugonjwa kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni, kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. Na mwisho ni kupata chanjo yake.tuzingatie pia usafi mashuleni, magerezani, makanisani, misikitini, day care ceners nk. Huu unaisha wenyewe na hauhitaji matibabu ya aina yeyote.ikitokea ukawa unahitaji dawa ni za kudhibiti dalili ulizo nazo tu (supportive treatments).  Jueni ya kwamba mgonjwa anapona kabisa ndani ya miezi 6 na anakua hana shida yeyote kama madhara ya HAV, ndo uzuri Wa kirusi hiki hua sio mbaya kama wenzake.  NAMNA YA KUJIKINGA  Njia kuu ya kujikinga na haya maambukizi ni kufuata njia bora za usafi kwa kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka chooni,kuosha mboga na matunda kabla ya kuyatumia, kupika vizuri mboga za majani na vyakula vingine kama samaki nk. na mwisho ni kupata chanjo yake, tuzingatie pia usafi mashuleni mag...